Ukistaajabu Ile Tattoo ‘Shishi baby’ kwa Mziwanda Jionee Hii ya ‘Irene Uwoya’ kwa Vjaymapenzi!


Katika hali ya kuonyesha hisia zake kwa staa wa bongo movies, Irene Uwoya kijana anayejiita Vjaymapenzi amejichora tattoo yenye jina la staa huyo  mkononi na kufunguka haya mtandaoni.

Itatokea kwa iman yenye uvumilivu wa wazi maana unaeza jizuia kwenda haja lakini sio kujizuia kumpenda mtu alitunukiwa ndani ya moyo wako na nafsi ikamkubali...ni rahisi sana kuwa tayara kwa lolote sababu chaguo la moyo ni chaguo la furaha na faraja ya maisha...kumpenda Irene Uwoya ni ugonjwa wangu na sijui kama nitapona sababu sina mpango wa kutafuta matibabu ni mie na yeye na yeye na mimi".

Uwoya naekupitia ukurasa mtandaoni alimjibu kwa “Asante sana kwa kunipenda Vjaymapenzi" mara baada ya kuweka picha ya Vjaymapenzi yenye tattoo na maelezo yake.

Hakika watu wanapenda jamani.

Mzee wa Ubuyu