Siasa yamtia Akili Baby Madaha..Amekata Shauri Kuachana na Skendo na Utoto ili.........


Baby Madaha Katika Pozi
BAADA ya kushuhudia wasanii wenzake wakijiingiza katika siasa na kuanguka, staa wa muziki na filamu, Baby Madaha ametia akili na kusema sasa atatulia kwani ni imani yake siku moja atajiingiza katika jukwaa hilo.

Alisema sasa ameamua kuachana na maisha ya skendo za kila siku kwani aliumizwa sana na madai ya kutumia dawa za kulevya, kitu kilichomuumiza hadi mama yake mzazi.

Ninajiandaa kuwa kiongozi wa kisiasa miaka ijayo, unajua hata wenzetu walioingia kugombea uongozi wa siasa na kushindwa, ilichangiwa na historia ya maisha yao ya kisanii, sisi ni watu wa skendo tu, nimejifunza kitu kutokana na hilo, nimeamua kuacha utoto, sitaki tena skendo,” alisema Baby Madaha.
Source:Globalpublishers
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI