Lulu Michael bado pepo la mahaba na Justine Beiber linamtesa,asema haya tena kwenye kurasa yake ya instagram....

Imekuwa sio siri tena Kwa Lulu kuvutiwa kimapenzi na mwimbaji ,wenye asili ya canada anayefanya kazi zake za ki muziki huko nchini marekani, suala la lulu kumzimia jamaa huyu ni miaka zaidi ya mitano sasa na ndilo jambo ambalo team ya Saa mbovu inaona sio la mzaha mzaha hata kidogo mana miaka 5 sasa kauli za lulu zipo pale pale akilia na penzi la beiber!!.
Kipindi cha nyuma mnamo mwezi wa nane tarehe 17 mwaka 2011 mtandao wa blog ya zamaradi mketema uliweka habari hii hapa chini.
Mwaka jana tu tena mtandao wa timesfm.com unaomilikiwa na radio times nao ukadondosha udambwi dambwi huo!! 
Siku nyingine tena mtandao wa bongo5 unaojihusisha na habari za burudani hapa nchini ukafunguka bila hiyana kuhusu saga hili.
 
Hii imefanya Saa Mbovu kufanya kiutafiti kidogo imegundua Lulu kaoza , akajifia na kujizika kabisa kwa kijana huyu mkali wa R&B mana imefikia hatua kaweka nadhiri kabisa kila jumatatu kupitia mtandao wake wa instagram ni spesho post kwa ajili ya justine beiber na jumatatu iliyopita hichi ndicho alicho post.

Huku akiandika "Uliamua kuni follow kwa Hiari Yako....vumilia Na Post Zangu Tafadhali" hii inatoka na wadau ambao ni follower wa kurasa yake kuwa wakichana mbaya kila akitupia vitu vya huyu jamaa kiasi cha kupelekea kuwa ambia watakoma naye na kula sana maliamo kama wanaona kichefu chefu na moyo wake ulipo dondokea!! hahahaha kweli hapa SAA MBOVU ISHAPOTEZA MAJIRA.