Katika hali isiyokuwa ya kawaida, watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino), 
wamepigana ngumi na mateke wakigombea kuingia kumwona Rais Jakaya 
Kikwete, Ikulu jijini Dar es Salaam. Tukio hilo la aina yake lilitokea 
jana majira ya saa nne asubuhi ambapo lilianzia kwenye eneo la mapokezi 
Ikulu mara baada ya walemavu hao kukaguliwa na kuwekwa kwenye chumba 
maalumu cha kupumzikia wageni. Baada ya muda, ofisa wa Ikulu alifika 
kwenye chumba walipokuwa walemavu hao akiwa na karatasi yenye orodha ya 
watu 15, ambao ndio waliopaswa kumwona Rais. Kila ofisa huyo alipokuwa 
akisoma jina, mhusika alitoka nje ya chumba hicho tayari kwa kwenda 
kumwona Rais. Baada ya ofisa huyo kumaliza kusoma majina hayo, alisema: 
“Hawa ndio wanaokwenda kuwawakilisha kwa sababu hamuwezi kuingia kundi 
lote hili.”
Wale wengine walioachwa hawakukubaliana na hali hiyo basi vurugu ndio likaanzia hapo!
Nini maoni yako kuhusu hili