“Tunaigiza filamu hakuna udhalilishaji lakini kuna Komedi tuliwahi kucheza ilikuwa inataka wasanii wa kike wawe na maumbile makubwa yaani makalio, kuchesha makalio sasa huo si uchekeshaji ni udhalilishaji, hicho ndio kilinifanya nichukie Komedi,”anasema Light.
Light anasema kuwa waandaaji wasiangalie tu maslahi yao tu pia waangalie waigizaji nao maisha yao baadae wakiwa na familia zao na wakiangalia filamu zao za Komedi zilizotolewa siku za nyuma watakuwa katika hali gani, hali ambayo inamfanya asipende kuigiza Komedi