Filamu za Kibongo za Zidi Kupasua Anga za Kimataifa! Soma Hii


Filamu za kitanzania maarufu kama Bongo Movies zimezidi kuvuka mipaka na kupata fursa ya kuonekana zaidi duniani.Hii ni kutokan na hiki ambacho blogger maarufu  Jestina George  mtanzania aneishi ughaibuni kushea nasi kile alichokutana nacho akiwa ndani ya ndege.

"I was very happy hivi karibuni wakati nasafiri ndani ya Emirates kukutana na hii .BongoMovie ..MkeMchafu humo ndani ninaemjua ni Johari Chagula pekee yake . but lengo lakuleta hapa ni kuwapongeza sana maana ni hatua nzuri and I hope tutaendelea kukutana na movie zingine pamoja na miziki yetu pia kwenye mashirika mengine ya ndege.. Kwani waowaweze sie tushindwe tuna nini"-  Jestina wa Jestina-george.com aliandika  mtandaoni  na kuwa tag baadhi ya wasanii wa bongo movies.

Hizi ni dalili nzuri, wasanii endeleni kukaza buti,wadau tuendelee kuwasapoti kwa kupenda vya kwetu