U HEARD INAYOMUHUSU WEMA NA SITTI MTEMVU HII HAPA!!


Soudy Brown leo katuletea U Heard inayowahusu Wema Sepetu na Sitti Mtemvu ambao waliwahi kuvaa Taji la Miss Tanzania kwa nyakati tofauti.

 
Soudy amewalinganisha Wema na Sitti kwamba, wakati ambao Wema alishinda
Taji hilo kulikuwa na story kwamba ameongopa umri kwa kujiongeza miaka miwili huku Sitti kukiwa na story ya kupunguza umri miaka miwili pia story ya kwamba wote walikuwa wanene.


Sitti Mtemvu baada ya kuvishwa Taji la Miss Tanzania 2014.Kuhusiana na Sitti kujivua Taji, Wema amesema kama ingekuwa ni yeye asingevua taji kutokana na mambo ambayo yalikuwa yakizungumzwa mitandaoni baada ya kuvishwa Taji hilo.