Kajala Awapoza Walioshindwa, Shindano la EFM


Staa wa Bongo Movies, Kajala Masanja hivi majuzi aliwapoza washiriki walioshindwa kwenye shindano la Shika Ndinga  lililoandaliwa na Kituo cha Redio cha EFM cha jijini Dar es Salaam.

Ambapo mkazi wa Ilala, Stela Robert (26) na Gabriel Geoffrey (36) wa Temeke wameibuka washindi wa gari na kukabidhiwa funguo za magari yao katika viwanja vya Tanganyika Pekas Kawe  ambapo lilifanyikia shindano hilo.

Kwa mujibu wa ofisa Uhusiano wa EFM, Lydia Moyo alisema shindano hilo lilikuwa na raundi nne ambapo washiriki walitakiwa washike kitu huku wakiwa wamesimama kwa miguu miwili, kisha wasimame kwa mguu mmoja na mwingine ukiwa umekunjwa kwa nyuma.

Alisema washiriki waliovumilia maumivu katika mizunguko hiyo minne walikuwa wawili ambao ndiyo walioibuka washindi ambapo mmoja kwa upande wa wanaume na mwingine kwa wanawake.

Kutokana na ugumu na shangamoto za shindano hilo akiwa ni moja kati ya waalikwa wa kwenye shindano hilo, Kajala Masanja ‘Kajala’ aliwapoza washiriki wote walioshindwa kushinda gari kwa kuwapa pole yake ya Sh 10,000 kila mmoja.