Lulu Michael Ahuzunishwa na Watu Wanao Mkejeli Kwa Kumhusisha na Kifo cha Komba

Habari kutoka kwa chanzo chetu ambacho ni mtu wa karibu wa Lulu, staa huyo alijikuta akiumia moyo kama walivyo binadamu wengine lakini hali hiyo imekuwa ikimtesa hasa aina ya meseji zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa mwanaume ‘akiwa karibu naye’ basi ajiandae kuaga dunia.

“Eti mwanaume kama ana jina linaloishia na ‘MBA’ kama Komba au Kanumba (marehemu steven Kanumba) basi imekula kwake,” kilisema chanzo hicho na kufafanua kwamba maneno hayo yameuchoma moyo wa Lulu kiasi kwamba anahitaji ushauri wa kisaikolojia.
Ilisemekana kwamba, hali hiyo imemkosesha raha Lulu na kuwaona baadhi ya Watanzania kuwa ni watu wasiojua maumivu ya moyo kwani naye ana moyo wa nyama na siyo chuma.
Chanzo hicho kilieleza kwamba, kwa umri wa Lulu wa miaka 20 amebebeshwa mzigo mzito mno hadi amefikia hatua ya kutamka waziwazi: “Watanzania imetosha, nimewakosea nini? Naombeni nihurumieni jamani!