Mahakama iliyoketi chini ya Jaji Mziray, ilikubaliana na hoja za mawakili wa Chadema, waliosema kuwa ufunguaji wa kesi hiyo ulikiuka baadhi ya vifungu vya sheria na hivyo kumtaka mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini kulipa gharama zote za kesi hiyo.
Baada ya hukumu hiyo, Zitto Kabwe amesema hakuwa na wito wa mahakamani leo na Jaji aliyekuwa akiisikiliza kesi hiyo amehamishiwa Tabora, hivyo mwanasheria wake ameenda kufuatilia mazingira ya hukumu hio.
"Hatuna taarifa ya Jaji Mpya. Mwanasheria wetu anafuatilia na atatoa statement", ameandika Zitto Kabwe katika ukurasa wake wa twitter.