Florah mbasha: Nipo Tayari Kurudiana na Mume Wangu.

Muimbaji wa muziki wa injili, florah mbasha amesema yupo tayari kurudiana na mume wake emmanuel mbasha, ikiwa atakwenda kumuangukia mguuni na kumuomba msamaha.

Florah alisema hayo alipozungumza na waandishi wa habari baada ya kumaliza kutoa ushahidi mahakamani juu ya kesi ya ubakaji inayomkabili mume wake ambayo inasikilizwa katika mahakama ya wilaya ya ilala.

"Mbasha nimeshamsamehe siku nyingi na nipo tayari kuishi naye iwapo atakuja kuniangukia miguuni na kuniomba msamaha..lakini hili la ubakaji ni suala la mahakama" Alisema.