Breaking News:Sigombei Uenyekiti ACT- Wazalendo Kama Wengi Walivyodhani-Zitto Kabwe

Aliyekuwa mbunge wa kigoma kaskazini Ndugu Zitto Kabwe 
amesema hatagombea nafasi ya Uenyekiti katika chama alichojiunga
nacho hivi karibuni cha ACT.
Amesema hayo muda mfupi kupitia redio E FM katika kipindi
katika mahojiano kinachoitwa 'Mezani'.
Zitto anasema tayari nafasi zote zimeshajazwa fomu na zimerudishwa tayari
na yeye hakujaza fomu za kugombea.
Anasema wote wale waliosema amekwenda ACT ili
awe kiongozi watakuwa wameumbuka