Taarifa zlizotufikia hivi punde ni kuwa moto mkubwa umezuka katika
Jengo B lililopo ndani ya Mabibo Hostel zinazomilikiwa na kuendeshwa na
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Shuhuda aliyekuwa eneo la tukio ametujuza kuwa Askari wa Zimamoto
wamechelewa kufika na athari zilishaanza kuwa kubwa, jitihada za kuuzima
moto huo zinaendelea.
Mtu mmoja ameumia kutokana na kuruka kutoka ghorofani