Mkuu wa Polisi wilaya ya Masasi, Azaria Makubi alisema inadaiwa alitenda kosa hilo juzi saa 9:00 katika kijiji cha Maili Sita huku bibi wa mtoto akiwa amekwenda nyumbani kwa mwalimu wa shule anakosoma mjukuu wake (aliyelawitiwa) kwa mazungumzo.
Alisema siku ya tukio mzee huyo alimkamata mjukuu wake na kumwingiza chooni huku akimweka vitambaa mdomoni asitoe sauti na alipomaliza kitendo chake hicho cha kinyama alimpatia mtoto Sh 2,000 ili asitoe siri kwa wazazi wake.
Inadaiwa watoto wenzake ndio waliotoa taarifa hiyo baada ya kushuhudia kitendo hicho kikifanyika na polisi kutaarifiwa.