Aunty Ezekiel alibandika picha hiyo hapo juu akiwa na jamaa kwenye ukurasa wake mtandaoni na kuandika maneno “My best friend,my love,my kimoko I love him so much”
Baada ya kubandika ujumbe huo baadhi ya mashabiki wake walionyeshwa kukerwa na mavazi na sehemu alikokuwepo nakumtaka atulie nyumbani alee mimba yake kwani kwasasa inaonekana kuwa na ya zaidi ya miezi nane na wiki kadhaa.
“Ungetulia tu nyumbani ukasubiri kujifungua salama,mjamzito kuzurura namna hiyo na mijanaume sio poa kabisa tena na kilaji mkononi harafu pia hata hayo mavazi mmmh!!” alisema mmoja wa shabiki na kuungwa mkono na wengine wengi.
Baada ya muda kidogo aunty ezekel akaibuka na kuandika ; “Plz msiwe bac mnaongea kitu kabla ujajua undani wake, ni vizuri kuuliza kuliko kuandika tu ilimradi na wewe uonekane umeongea hiyo nguo ni special kwa mama mjamzito na hapo juu inampira wakutosha tu na mapajani ndio inabana sasa”
Lakini majibu hayo yalionekana kuamsha maneno zaidi ya kumponda Aunty ambae nae mwishoni alionekana kushindwa kuvumilia na kutoa matusi mazito ambayo sio busara kuyabandika hapa.