"Kwanza wanaohangaika na CV za mavyuo ni wale wanaotaka kuwavutia wenye akili(waajiri) ili wawaelekeze cha kufanya(yaani wawaajiri). Mtu mwenye maono ya kujiajiri hahangaiki na CV za mavyuo bali anaangalia maarifa ya kumsaidia na kimsingi anaweza hata asiende shule bali akayapata maarifa hata mtaani tu". Akaniuliza, "Unamaanisha nini?" Nikamwambia, "Umesoma chuo Kikubwa lakini bado una akili za kikoloni zinazowaza kuwa hakuna maisha ya maana mpaka uajiriwe. Kusoma ni jambo zuri na kuajiriwa sio jambo baya lakini usikariri kuwa hakuna maisha pasipo kuajiriwa; na usifikiri kila anaefika chuo kikuu anawaza kuajiriwa tu. Siku hizi mafanikio kimaisha hayamo katika CV ya chuo ulichosoma na kamwe hutatajirika (au atleast kuwa na pesa za maana) kwa kutegemea mshahara pekee". Ikiwa imepita miaka sita sasa, sijajua hali ya kiuchumi na kimaisha ya yule brother; lakini ikiwa hajabadilisha ile "mentality" nina uhakika atakuwa "ni mbangaizaji tu" kiuchumi na kimaisha kwa ujumla licha ya kuwa anamiliki cheti cha digrii kutoka Makerere!
By Albert Nyaluke Sanga