Ikulu: Rais Kikwete akutana na Viongozi wa Chama cha Albino Tanzania

Katika hotuba ya Mwisho wa Mwezi wa Februari, Rais Kikwete aliahidi kukutana na Viongozi wa Chama Cha Albino Tanzania ili aweze kusikiliza kilio Chao na washauriane namna ya kufanya ili kukabiliana na mauaji ya Albino yanayoendelea Tanzania.

Dr Possy akimsomea Rais Kikwete Mapendekezo ya ​ Viongozi wa Chama Cha Albino Tanzania juu ya namna ya kupambana na kukomesha ukatili na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi nchini​

Rais Kikwete akiongea na ​Viongozi wa Chama Cha Albino Tanzania Ikulu jijini Dar es salaam leo Alhamisi Machi 5, 2015 alipowakaribisha ili kusikiliza matatizo yao na kujadiliana nao mikakati ya namna ya kukomesha ukatili na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi nchini​