TUMUOMBEE! Afya ya mama mzazi wa msanii nyota wa Bongo Fleva, Nasibu
Abdul ‘Diamond Platinumz, Sanura Kassim ‘Sandra’ bado si shwari juzikati
hali yake ilibadilika ghafla na kuilazimu familia yake kumkimbiza
katika Hospitali ya TMJ iliyoko Mikocheni jijini Dar ambako amepewa
kitanda, Ijumaa limetonywa.
Diamond alipotafutwa kuzungumzia afya ya mama yake aligoma kusema lolote
zaidi ya kuomba aachwe kwani wanao uwezo wa kuzungumzia mambo mengine
bila kugusia kuhusu mzazi wake.“Naomba unipe muda maana nina matatizo
sana, hata kuzungumzia ishu hiyo nadhani hakuna haja,” alisema Diamond.