Bondia Mohamed Matumla amemchapa mpinzani wake raia wa China, Wang Xin
Hua kwa pointi. Matumla ameshinda pambano hilo la kuwania ubingwa wa
dunia wa WBF la raundi 12 uzani wa Bantam lililopigwa katika Ukumbi wa
Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam usiku huu.