Lile gari jipya aina ya Nissan Murano
la staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ alilompa
aliyekuwa mwandani wake, Gorgeous Onyinye, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’
limezua mapya ambapo baada ya kudai linamchefua sasa anadaiwa kuwa
analiuza kwa kigezo kwamba hataki gundu mwaka huu mpya wa 2015. Inasemekana kwa sasa gari lipo kwa
dalali analitafutia mteja wa fasta fasta as Wema Hataki Kulisikia kabisa
wala kulitia machoni.