H-Baba Afunguka Kuhusu Kumwekea Bleach Kichwani Mtoto Wake, Adai Lazima Aishii Kistaa Kama Wazazi Wake


H-Baba asema lazima mwanaye aishi kisanii kama wazazi wake,afunguka kuhusu kumuweka 'bleach'
Msanii wa bongo Fleva,H: Baba amewafungukia mashabiki wake waliomjia juu baada ya kumuweka dawa ya nywele'bleach' mtoto wake,Tanzanite mwenye umri wa mwaka mmoja.
Mashabiki walimwambia msanii huyo kuwa bleach siyo nzuri kiafya kwa mtoto huyo,H: Baba akijibu tuhuma hizo alisema kuwa lazima mwanaye aishi kisanii kama wazazi wake na kwamba yeye kama mzazi hawezi kumuharibu mtoto wake.
'Watu wanashindwa kuelewa mimi sijampaka mwanangu bleach hiyo ni hina pia hina ni suna kwa dini yetu ya Kiislam sioni tatizo hapo,'alisema H: Baba.